Popular Posts

Popular Posts

Popular Posts

Popular Posts

Search This Blog

Popular Posts

Popular Posts

Saturday, February 28, 2015

TID AUPONDA VIBAYA WIMBO MPYA WA ALI KIBA CHEKECHA CHEKETUA.

Msanii wa Bongo Top in Dar maarufu kama TID au mnyamaa kupitia akaunti yake ya instagram ameuoponda vibaya wimbo mpya wa Ali Kiba,alioutambulisha Jana kwa jina CHEKECHA CHEKETUA.

Amesema nyimbo hiyo haitodumu ata miezi mitatu kwenye soko la mziki nchini..

Soma hapa:
"This song is not all that but u guys are making it a big sh**t,its gonna last 3 months, #nose singing."

DIAMOND AZIDI KUNG'ARA KIMATAIFA BAADA YA KUTANGAZWA KUWANIA TUZO YA MWANAMZIKI BORA WA AFRIKA NCHINI GHANA.

Majina ya wasanii watakao wania tuzo hizo yametangazwa jana Ijumaa tarehe 27,kwenye hoteli ya kifahari jijiini Accra Ghana inayoitwa PALM ROYAL BEACH HOTEL.

Diamond Platnumz ametajwa kuwania tuzo hizo kwenye kipengere cha Msanii bora wa Afrika ( African artist of the year)

Wasanii wengine wanaowania kipengele  hicho ni Tiwa Savage (Nigeria), AKA (South Africa),Don jazy & the mavn Group (Nigeria) na Yemi Alade (Nigeria).

Kupatikana kwa mshindi wa Tuzo hizo inatoka na 40% kutoka kwenye kura za wananchi,30% zinatoka kwenye Academy na 30% zinatoka kwa majaji.

Friday, February 27, 2015

KOBE 250 WAKAMATWA UWANJA WA NDEGE ZANZIBAR WAKITOROSHWA KWENDA MALAYSIA.

Kobe wadogo 250, wamekamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Aman Karume,wakiwa njiani kusafirishwa kwa njia ya magendo kwenda Malaysia.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Mk Adam Khamis Mk Adam,alisema kobe hao walikamatwa  wakiwa wamehifadhiwa katika masaduku yaliyowekwa maembe ndani yake,katika hatua za mwisho za kusafirishwa.

"Ni kweli tumekamata Kobe 250 wakiwa wamehifsdhiwa vizuri  katika masanduku yakiwa yameingizwa maembe tayari kusafirishwa kwenda Malaysia" alisema.

Hata hivyo Kamanda Hamdani alikataaa kumtaja mtu aliyekamatwa na kobe halo kwa madai kwamba uchunguzi unaendelea na kitendo cha kumtaja moja moja,kinawez kuharibu  uchunguzi wa tukio hilo.

"Jeshi la Polisi kwa sasa halipo tayari kumtaja mtuhumiwa aliyekamatwa na Kobe hao kwa sababu za uchunguzi zaidu unaendelea....unajuwa ukianza kuntaja mtuhuniwa pamoja na wangu wengine,unaharibu uchunguzi mzima wa tukio hilo" Alisema.

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na matukio ya wizi wa Kobe kutoka Zanzibar kupelekwa sehemu nyingine duniani ikiwa ni pamoja na Tanzania Bara.

Kobe hao wanalindwa na sheria za Kimataifa,wakiwa katika orodha ya viumbe ambao wapo katika hatari ya kutoweka duniani,kama ilivyo kwa sasa kwa hivyo wamekuwa katika udhibiti mkubwa.

Kwa upande wa Zanzibar,Kobe  wanahifadhiwa katika kisiwa kidogo cha Chum be kilichopp nje ya Bandari ya Malindi  umbali wa kilomita 40,ambapo hata hi yo kumekuwepo matukio ya wizi wa mara kwa mara.

Ofisa mmoja kutoka Kamisheni ya Utalii Zanzibar, ambaye moja ya majukumu yake ni kulinda na kuhifadhi Kobe waliopo  katika kisiwa kidogo cha changu,alikiri kuwepo wizi katika nyakati  tofauti,unaofanywa na watu wasiokuwa waaminifu wanaotembelea kisiwa hicho cha shuguli za utalii.

"Yapo matukio ya Wizi wa Kobe katika kisiwa cha changu kwa nyakati tofauti,kwani watu hufika katika kisiwa kwa shughuli tofauti ikiwemo za matembezi"alisema.

Katika miaka kumi iliyopita,zaidi ya Kobe 1,500 wameibiea katika kisiwa cha changuu,wakiwemo Kobe wadogo wanao hifadhiwa sehemu maalumu.

KIJANA AKANA KUBAKA NA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI WA MIAKA 16

Mkazi wa Tabata,Erasto Clement (22) amepandiswa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala na kukana mashitaka ya kubaka na kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato ya kubaka na kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha tatu mwenyewe  umri wa miaka 16.

Akisomewa  maelezo ya awali jana, wakili wa serikali Fosta Mosha alidai mbele ya Hakimy Mkazi Mwandamizi, Juma Hassan Kuwa katika tarehe na mwezi usiofahamika,mwaka jana,Clement pamoja na mlalamikaji walidaiwa kuwa wanafamiana kwa muda mrefu.

Mosha alidai kuwa septemba,2013 mshitakiwa na mlalamikaji waliamza mahusiano ya kimapenzi na kumuingilia kimwili mlalamikaji huyo huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Pia alieleza kuwa mlalamikaji  aliripoti taarifa hizo kituo cha polisi na kupewa  PF3 kwa ajili ya kwenda hospitali.

Wakili Misha alidai kuwa mlalamikaji alipofika hospitali alipimwa na kukutwa na ujauzito wa  miezi 6.

Mshitakiwa alikubali maelezo binafsi pia alikana kufikishwa mahakamani hapo kusomewa mashitaka yanayomkabili.

Hata hivyo,upande wa jamhuri ulidai kuwa utakuwa na mashahidi manne na kielezo kimoja ambacho ni PF3.

Hakimu Hassan aliahirisha kesi hiyo had I April mosi mwaka huu itakapoanza kusikilizwa.

DOWNLOAD WIMBO MPYA WA ALI KIBA "CHEKECHA CHEKETUA"

Ali Kiba ametoa single yake mpya leo inayoitwa CHEKECHA CHEKETUA,KUWA WAKWANZA KUSIKILIZA HAPA.

BREAKING NEWS:NDEGE YA JESHI YAANGUKA NA KUWAKA MOTO JIJINI MWANZA ..RUBANI ANUSURIKA

Ndege ya Kijeshi imeanguka Leo uwanja wa ndege wa Mwanza na kuwaka moto wakati inatoma kaskazini mwa uwanja huo kuelekea kusini ambapo rubani wake,Peter Augustino Lyamunda amevunjika mguu.

Chanzo cha ajali hiyo ni ndege (mnyama)  aliyeingia kwenye moja ya injini za ndege hiyo hiyo ilipotaka kuruka,ikashindwa na kuanguka.

DIAMOND KUTOA VIDEO MPYA WIKI IJAYO,ALIYOIFANYA KWA DIRECTOR MPYA WA BONGO ANAEKUJA JUU KWA SASA HANSCAN

Maneno yaliyosemwa na director mkenya Kevin Bosco mwanzoni mwa mwaka huu ( Hanscana is the director to watch) kuhusu director mpya kwa sasa,Hanscana yanazidi kutimia.

Baada ya kutisha na video mpya ya Barnaba na Vanessa Mdee,sasa Hanscana amepata shavu la kushoot video mpya ya Diamond Platinumz.

Kupitia kipindi cha "Clouds E" cha Clouds TV,kimeoneshwa kipande kidogo cha  wakati wa  utengenezwaji wa video (BTS)  ya wimbo mpya wa Diamond na Khadija Kopa ambayo kwa mujibu wa chanzo chao imefanyika Dar na Zanzibar. Video hiyo inatarajiwa kutoka wiki moja kuanzia sasa.

Diamond kuamua kufanya kazi na Director mpya ambaye anaonekana kukua kwa kasi,Hanscana ni ishara ya kuwa  ameamini uwezo wake kupitia video chache ambazo tayari ametoa.

Itakumbukwa kuwa baada ya Diamond kufanya kazi na Producer wa audio Shed Clever ndipo mila go mingi ya mafanikio ilifunguka kwa producer huyo  kutokana na kupewa njia na staa huyo..

Video zingine ambazo Hanscana amefanya no
Moyoni- Navy Kenzo
Siri- Vanessa mdee & Barnabas
Morale - G nako

DIAMOND NA AY WAMEKAMATA #1 KWENYE TOP 10 ZA MUZIKI WA AFRIKA ZA TRACE INTERNATIONAL NA SOUNDCITY..

Muziki wa Tanzania upo mahali pazuri kwa sasa. AY,Diamond Platnumz na wasanii wengine wanaiwakilisha vyema nchi yetu kimataifa.

Wasanii hao wamekamata nafasi za kwanza wiki kwenye top ten za chart za muziki wa Afrika katika vituo viwili vikubwa vya runinga.

Diamond Platnumz amekamata nafasi ya kwanza kwenye African Top 10 ya Trace International na wimbo wake wa  NTAMPATA WAPI.

Naye AY amekamata nafasi ya kwanza kwenye chart ya Africa Rox countdown ya Soundcity kwa wimbo wa "Touch Me" aliyomshirikisha Sean Kingston na Ms Triniti

Wasanii engine wa Tanzania waliopo kwenye chart hiyo ni pamoja na Navy Kenzo na Shaaa.

Thursday, February 26, 2015

TEAM WEMA WALIMPUA ZARI THE LADY BOSS KWA KURUDIA NGUO MOJA KILA WAKATI KATIKA MITOKO TOFAUTI.

Page moja huko instagram inayojiita Wemaselfies wamemlipua Zari kwa kusema anarudia nguo moja kila wakati katika mitoko tofauti.. Jisomee hapa

"Hivi hiyi tyt hayibadilishwi? Khaa jaman sasa Bosslady gani anavaa the same thing kila siku? Wewe mama uliingiana gia ya 5 sasa utatoka without no gia hivi nyiye Domo mnamuelewe kweli?
Mie mnisaidie nikwanini akiwa na mwanamke lazima huo mwanamkr ajisahau Sari stop your stupidity ndkuona unavyo comment kwa lemapumbuz ww jobless don't try os ooh a beg and nyie team Zari soon mtaanza kampeni bring back zari if not ooohhoo mamkubwa kapotea yaani Zari  Kwisha no big big money no job no nothing ww acha kufatilia team wema plzzz ooh. May Allah bless my @wemasepetu katika kila kitu anachofanya asante mungu kuona kakuamsha mapema  kwenye usingizi  najua wengine hivi walipo wanapanga tufanye mini ili tumuharibie wema but nothing to worry mungu yuko na ww @wemaseptu wangu we love u and wish u all the best "

RAY C ACHAFUKWA AWAFUNGUKIWA TEAM WEMA "WAENDE ZAO WASITULETEE SHOBO HAPA TEAM USHUZI TEAM NJEGERE"

Kitendo cha Ray C kumshauri Diamond amuoe Zari the Boss Lady kupitia mtandao wa instagram watu mbalimbali  ambao ni mashabiki wa Wema walianza mtukana Ray C kwa vijimaneno vya hapa na pale kitu ambacho Ray C hakukipenda  na kuamua kuwashukia na kuwapa soma ifuatayo:

"Waende zao wasituletee shobo hapa Team Ushuzi Team Njegere,I don't give Fuc.kin care! Mi mwenyewe nimetoka lutindi! wanajifanya vichaa simu zetu vidole vyetu vocha tunanunua wenyewe halafu tuogope kucomment  kwa msanii mwenzetu eti kisa wao hawapendi kwani waneninulia simu au siwezi nyimwa Uhuru wa simu yangu kwa sababu ya wajinga wasiosoma! Mtu mwenyewe kukaa insta Massa 24 huyo hana kazi! Wafanya insta kama kariakoo...Mnaojifanta mnahua kutujana wejeni sura zenu tuwaone.......Ray C_

   In three words I can sum up everything, I've learned about life:it goes on.

LIVERPOOL NA TOTTENHAM ZATUPWA NJE LIGI YA EUROPA. EVERTON YAENDELEZA UBABE,PATA MATOKEO ZA MECHI ZINGINE HAPA YA EUROPA

Jana Liverpool ilijikuta ikitolewa katika michuano hiyo ya ulaya maarufu kama EUROPA kwa njia ya mikwaju ya penati baada mechi kumalizika kwa Liverpool kufungwa mmoja bila. Kwa matokeo hayo ikafanya kuwa ni Besktas 1 vs 1 Liverpool,kutokana  na Liverpool kushinda gori moja mechi iliyopita.
Liverpool walipata penati 4 wakati Besktas wakipata zote 5. Kwa matokeo hayo Liverpool imeondolewa kwenye mashindano.

MATOKEO ZA MECHI ZINGINE.

FORENTINA 2- 0 TOTTENHAM (3-1)
INTER 1- 0 CELTIC aggregate (4-3)
Everton 3- 1 YOUNG BOYS (7-2)
FEYENOORD 1- 2 ROMA
NAPOLI 1-0. TRABZNSPOR
SPORTING. 0-0 WOLFSBURG
GLADBACH 2- 4 SEVILLA

WATU 3 WATEKETEA KWA MOTO BAADA YA LORI LA MAFUTA KUPINDUKA NA KUWAKA MOTO

Watu watatu wamefariki dunia kwa kuungua moto kuteketea kabisa akiwemo dereva na utingo wale baada ya Lori la mafuta kuacha njia na kupinduka na kuungua moto katika eneo LA Maseyu Barbara ya Morogoro Dar es Salaam.

Mwandishi wetu alishuhudia kikosi cha zimamoto ambao wakichukua muda kuuzima huo moto kutokana na kusambaa ambapo hata hi yo hakukua na matukio ya wangu kujitojeza kuiba mafuta kama ilivyozoeleka.

Baada ya kumaliza kuuzima moto huo kikosi cha zimamoto na uokoaji wakafanya juhudi nyingine za kuvuta kwa craine na kukata kwa kutumia mashoka mabaki ya Lori  hilo baada  ya walioshuhudia tukio. Kueleza kuwa gari hawakutoka ambapo baada ya muda miili mitatu iliokolewa ikiwa imeungua kabisa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wakiwemo madereva wa malori ambapo walukuwa wakisafirisha mafuta katika kampuni moja Farhan Yusuf  amesema Lori hilo lilikuwa lumesheheni mafuta ya Dezel mali ya kampuni ya Petrol Africa ilikuea ikitokea Dar es salaam kwenda jijini Mwanza ambapo ilipoteza muelekeo na kupinduka Kisha kuwaka moto.

Waliofariki dunia ni Ahmed Dilie dereva na utingo wake aliyefahamika kwa majina ya Emela na mtu mmoja ambaye hakuweza fahamika mara moja.

Nao wananchi walioshuhudia tukio hill wameeleza jinsi tukio lilivyotokea ambapo wananchi wanelalamika eneo hilo kuwa limekuwa na matukio mengi ya ajali na hivyo kuomba serikali kuona umuhimu kuweka vituo vya zima moto katika eneo hilo kwani magari ya zimamoto yalichukua muda mrefu kufika kwenye eneo la tukio kutokana na umbali mrefu.

Nae Afisa mkaguzi msaidizi wa kikosi cha zima moto Hamadi Dadi ameeleza walivyopata taarifa za ajali wametumia muda mrefu kufika katika eneo hilo la tukio,ingawa wametumia muda mrefu kuuzima huo moto kutokana na mafuta yaliyokuwa yakivuja.

Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo,na askari walionekana muda wote kwenye eneo la tukio.

PICHA YA MPENZI WAKE DIAMOND, ZARI AKIOGA BAFUNI YAZUA GUMZO MTANDAONI.

Picha ya mpenzi wa staa wa Bongo Fleva,Diamond Platnumz,Sari  aliyoipost kwenye akaunti yake ya instagram akiwa kwenye bafu akioga imezua gumzo kwenye mitandao huku engine wanasema kuwa hakupaswa kuweka picha ile na kwamba amejianika hana maadili.

Haya ni baadhi ya maini ya mashabiki wakizungumzia picha hiyo.

faridahfakhi: Noo kinachotia kinyaa ni kwamba haikupaswa ajianike apo ili iweje istoshe kamera zinawastili watu .

WAKAZI WA ILULA MKOANI IRINGA WAGOMA KUPOKEA MAITI ALIYEUAWA NA POLISI.

Wakazi wa Ilula Mkoani Iringa wamegoma kupokea maiti ya mama aliyekuwa wakati wa mapambano yaliyotokea juzi mkoani humo kati yao na Polisi kwa masharti mawili.

MOSI : Wananchi 18 waliokamatwa na Jeshi la Polisi baada ya vurugu hizo waachiwe huru Mara moja bila  masharti yoyote.

PILI: Polisi walio sababisha mauaji hao wakamatwe na kufikishwa mbele ya sheria.

Katika tukio hilo wananchi wa ilula walimtuhunu polis I kumuua mwanamke kwa kosa la kuuza pombe muda wa kazi na hivyo kupanda gadhabu na kuvamia kituo cha polisi ambako walichoma magari matano madogo na basi moja na baadae kwenda kufunga Barabara ya Dar es Salaam - Mbeya kwa muda wa masaa 5.

ALLAN KINGDOM: RAPPER MTANZANIA ALIYESHIRIKISHWA NA KANYE WEST KWENYE NGOMA MPYA 'ALL DAY'(DETAILS)

Kanye west anafahamika kwa kuwatoa wasanii wangu wakubwa nchini Marekani.Bila yeye leo hii hakuna mtu angekuwa anawajua Big Sean na John Legend. Na sasa kupitia ngoma yake mpya 'all day' (ambayo hakuna shaka itakuwemo kwenye album yake mpya),yeezy anamweka kwenye ramani ya muziki duniani,rapper Mtanzania aishie Minnesota,Marekani Allan Kingdom.

Hakuna mkazi wa Minnesota asiyemjua rapper huyu na infact ni superstar tayari pande hizo japo tunasikitika kuwa tumemfahamu sasa kupitia Kanye West aliyemshirikisha kwenye ngoma yake ambayo tayari inapendwa na ilivuja wiki iliyopita.

Kinachotufurahisha zaidi ni kuwa Kanye amempandisha rapper huyo jana (jumatano)kwenye Brit Awards (zenye level sawa na tuzo za Grammy za Marekani)zilizofanyika jijini London kutumbuiza ngoma hiyo.

Kwa mujibu wa Star Tribune,Kanye atakuwa amemfahamu Allan kupitia mkurugenzi wake wa ubunifu, Virgil Abloh ambaye ni sehemu ya watu walio kwenye kambi ya Allan. Hakitakiwa kitu cha ajabu kama akishawishika pia kumeongeza kwenye list ya wasanii wa lebo yake,GOOD MUSIC.

ALLAN KINGDOM NI NANI?
Mwaka jana mtandao wa komplex ulimjumuisha kwenye orodha ya rappers 25 wapya wa kuwaangalia mwaka 2014. Allan Kingdom ni rapper na producer wa musiki mwenye makazi yake St paul ,Minnesota nchini Marekani.

Alizaliwa kwa jina la Allan Kyaringa miaka 21 iliyopita nchini Kanada na mama yake kutoka Tanzania na baba kutoka Afrika kusini.

"Naweza kuzoea kiurahisi kabisa kwenye mazingira tofautitofaiti, lakini sijawahi kuhisi kiukweli kuwa Mimi ni sehemu ya jamii moja". Rapper huyo aliliambia gazeti kubwa zaidi la kila siku katika jumbo la Minnesota,Star tribune.

Mtindo wake wa muziki unachukua sana vionjo pia kutoka Afrika Mashariki kupitia muziki ambao mama yake alikuwa akiskiliza alipokuwa mdogo na kuchanganya na ladha za waimbaji wanaomuenspire kama Frank Ocean Odd Future,Earl Sweatshirt na Kid Cudi.

Uhusiano wake na Kidd Cud ni mkubwa zaidi kwa kuwa mmoja wa watayarishaji wa Cud,Plain Pat ni meneja wa Allan.

"Aliniambia nimetishwa sana na production yako,"Pat anamkumbushia Allani ambaye kipindi hicho alikuwa na miaka 17 kupitia Twitter.

Akiwa mtoto wa pekee wa wazazi wake,ametumia mda mchache mno kukaa na baba mtoto aliyerudi Afrika kusini wakati Allan akiwa mtoto. Kwa hiyo amelelewa zaidi na mama yake Mtanzania.

Wazazi wake walikutana wakati skiwa wanasomo kwenye chuo kikuu cha Manitoba, huko winnipeg nchini Canada na aliishi huko hadi darasa la 3.
Mama yake Laurentian aliwahi kumleta Tanzania mara kadhaa na kumfundisha utamaduni wa nyumbani.

Akiwataja wasanii wakongo kama vile Koffi olomide,Papa wemba,Allan alisema
  "Mwanzoni nilipoanza kutoa nyimbo watu walisema walikuwa wakisikia hiyo 'influence' na kwakweli kilikuwa ni kitu kinachotokea bila kujua (subconscious). Lakini nilifikiria,'ok, basi naweza kuimiliki pia. Na ndipo nikaanza kusikiliza nyimbo hizo Mimi mwenyewe."

Ushawishi kutoka kwa mtengenezaji wa nyimbo za Kanye unasikika kwenye EP yake ya miaka miwili iliyopita,trucker music iliyodhihirisha kipaji kilichopevuka katika umri wake mdogo.

Akiongea na Papermag.com mwaka jana,Allan alisema  Minnesota ni sehemu yenye wahamiaji wengi wakigeni kutoka Afrika Mashariki na hivyo kumfanya kujisikia yupo nyumbani.

"Ninaweza kusimama sehemu na kupata kitu kinacho fanana na kile mama yangu angetengeneza,"alisema.

Kazi yake mpya inaitwa Future Memories yenye jumla nyimbo 12  zikiwemo Wavey na  Evergreen.

WIMBO MPYA YA ALI KIBA INAYOITWA "CHEKECHA" KUTOKA KESHO IJUMAA.

Msanii alietamba kwa muda mrefu na ngoma yake Mwana ,Ali Kiba kesho anatarajia kutoa wimbo yake  mpya unaokwenda kwa jina la CHEKECHA,kupitia ukurasa wake wa Instagram  baada ya kuonesha ujio wake mpya wa mashabiki wa Ali Kiba.

Ali kiba aliachia nyimbo zake mbili kimasomaso na Mwana 25/7/2014  baada ya kimya cha mda mrefu baadae kuna nyimbo mbili zilitoka ambazo kwa mujibu wa Ali Kiba alidai kuwa hakuzitoa bali zimevuja.

Je ujio mpya wa Chekecha utakuwa mkali zaid ya Mwana?

BREAKING NEWS: CHIDI BENZI AHUKUMIEA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI JELA:

Mwanamziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Rashid Abdalah Makwaro maarufu kama (Chidi Benzi) amehukumiwa  kifungo cha miaka miwili  jela au kulipa faini ya shilingi 900000 kwa kosa la kutumia madawa ya kulevya na bangi.

Chidi Benzi alikamatwa uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam,akiwa na madawa ya kulevya aina ya Heroin yenye thamani ya 38000,bangi zenye thamani ya 1700, pamoja na vifaa vya kutumia madawa ayo.

Chidi Benzi alikiri kosa mbele ya mahakama kuwa ni mtumiaji wa madawa hayo. Baada ya mahakama kusikiliza pande zote mbili ikamkuta Chidi Benzi ana hatia na kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Tsh900,000/=

Wimbi la wasanii wanaotumia madawa ya kulevya linazidi ongezeka,nguvu kazi za taifa zinazidi kupotea lakini hii yote inasababishwa na waingizaji na wasabazaji wa haya madawa nchini

MAIMARTHA AMWEKA KITI MOTO AUNTY LULU KUHUSU KULALA GESTI NA KUTOKA NA WANAUME WASIO NA MAANA MJINI.

Mtangazaji maarufu wa Runninga Maimartha Jesse hivi karibuni aliamua kumtolea uvivu,Lulu Semagongo 'Aunty Lulu' kwa kumpiga kitchen party ya nguvu.

Akichonga na centre spread,Mai alisema Kuwa anachoumia ni kwamba kila mtu mjini hapa anamsema Lulu vibaya wakati yeye alikuwa rafiki yake wa karibu.

"Kama atalia na alie,kama atacheka na acheke lakini nimeshachoka na mambo yake kwa sababu yeye ni uzima kichwa,anasumbua vichwa vya watu kwa matendo yake" alisema Mai.

Aidha, Mai alisema anamsema lulu kama mdogo wake na mtu aliyemfanya akapata Jina mjini hapa kuwa aache Tabia ya kulala gesti na kuwa karibu na wanaume wasio riziki.

FILAMU ZA KIBONGO ZA ZIDI KUPASUA ANGA ZA KIMATAIFA:SOMA HII.

Filamu za kitanzania maarufu kama Bongo Movies zimezidi kuvuka mipaka na kupata fursa ya kuonekana zaidi duniani.Hii ni kutokana na hiki ambacho Blogger maarufu Jestina George mtanzania aneishi ughaibuni kushea nasi kile alichokutana nacho kwenye ndege.

"I was very happy hivi karibuni wakati nasafiri ndani ya Emirates kukutana na hii Bongo Movie... MkeMchafu humo ndani ninayemjua ni Johari Chagula pekee yake. But lengo lakuleta hapa ni kuwapongeza sana maana ni hatua nzuri and I hope tutaendelea kujutana na muvi zingine pamoja na miziki yetu pia kwenye mashirika mengine ya ndege. Kwani wao waweze sie tushindwe tuna nini"- Jestina-george.com aliandika mtandaoni na kuwatag baadhi ya bongo movies.

Hizi ni dalili nzuri,wasanii endeleeni kukaza buti,wadau tuendelee kuwasapoti kwa kupenda vya kwetu.

Wednesday, February 25, 2015

JB NA SCANDAL MPYA NDANI YA BONGO MOVIES:

Msanii anayefanya vizuri kunako bongo movie, Jacob Steven maarufu kama  JB, hivi karibuni amejwaa scandal mpya ambayo inamshushia heshima kama sio kumpunguzia credit ndani ya tasnia hiyo.

Msanii huyo maarufu amekumbwa na skendo hiyo baada ya muvi yake mpya kutoka inayifahamika kwa jina la MZEE WA SWAGA.

Muvi hiyo inayofanya vizuri sokoni inasadikiwa kukopiwa na kupesti  kama ilivyo na moja ya muvi maarufu kutoka Bollywood inayofahamima kwa jina la "LADIES VS RICKY BAHL".

Akizungumza kupita kipindi cha take one,Zamaradi Mketena amethibitisha usanii huo uliofanyika na kampuni maarufu ya JERUSALEM inayomilikiwa na JB,kuwa karibia scene zote zilizochezwa na Filamu ya Mzee wa swaga, imeiga kama ilivyo kuanzia stori hadi idadi ya waigizaji wakuu kutoka kwenye filamu hiyo ya kihindi iliyotoka mwaka 2011.

Mtangazaji huyo amelaani vikali utapeli huo uliofanyika na kampuni ya JB huku akijifanya yeye ndo mtunzi na mwandishi wa stori hiyo wakati ukweli anaujua mwenyewe.

SHILOLE ATAJA CHANZO CHA MIGOGORO NA NUH MZIWANDA.

Mwanamziki na mwigizaji wa filamu za Bongo, Zuwena Mohammad 'Shilole' ameamua kuweka wazi chanzo cha migogoro yake na mumewe mtarajiwa,Nuh Mziwanda kuwa ni marafiki.

Shilole alidai kuwa mara nyingi wamekuwa wakigombana,lakini chanzo kikiwa ni maneno ya uchonganushi kutoka kwa marafiki zao wa karibu ambao wanalengo wana lengo la kuwatenganisha. Mwanadada huyo alidai kutokana na hali hiyo hivi sasa ameamua kuowahusisha suala lolote linalohusu maisha yake ili kupubguza migogori ya mara kwa mara baina yao.

Alisema wale walio karibu yao ndio  wanaochangia kwa kasi kikubwa kutokea kwa migogori kwenye mahusiano yao,ukizingatiwa hivi sasa wapo kwenye harakati za kufunga ndoa baada ya wazazi wa pande zote kukubali uhusiano wao.

"Tumegundua kuwa mashoga ndio wanaotugombanidha,kwani kila mara mchumba wangu anapewa taarifa zinazonihusu mimi huku hao hao wananiletea habari zake,jambo chili limesababisha nisiihitaji tena marafiki wengi wao ni wanafiki" alisema.

ARSENAL NJE LIGI YA MABINGWA ULAYA,BAADA YA KUPIGWA 3 NA MONACO;BAYERN LEVERKUSEN YAIADHIBU ATLETICO MADRID KIMOJA TU.

Mashabiki wa Arsenal jana ilikuwa siku chungu kwao baada ya kuishuhudia timu yao ikipigwa kipigo kitakatifu na timu ya Monaco inayoshiriki ligi kuu Ufaransa.

Mpaka mpira unamalizika matokeo yalikuwa ni Arsenal 1 vs 3 Monaco. Safu ya ulinzi wa Arsenal ilikuwa mbovu zaidi iliyomfanya nyota wa zamani wa Manchester United kuonekana mwiba wa kuotea mbali kwa kuisumbua sana ngome ya Arsenal

Wenger aliwahi kuifundsha Monaco kwa miaka 7 na kuiwezesha timu hiyo kuchukua vikombe vya ligi kuu ya Ufaransa,na UEFA CUP.Wenger aliikacha timu hiyo na kujiunga na washika bunduki wa London.

Arsenal itakuwa mara ya kwanza kutoka kwenye hatua ya 16 bora ya UEFA tangu mwaka 2010.

KIKOSI CHA ARSENAL.
Mfumi:4-4-2.
Ospina,Bellein,Mertasacker,Koscielny,Gibbs,Coquelin,Cazorla,Sanchez,Ozil,Welbek(chamberlain),Giroud.

Goli: Chamberlain 90+1 dakika.

KIKOSI CHA MONACO.
Mfumo:4-5-1.
Subasic,Toure,Wallace,Abde,Eldeson,Dirar,Kondogbia,Fabinho,Moutinho,Martial,Berbatov.

Goli.  Kondogbia 38dk
          Berbatov.   57dk
          Else son.    90+4 dk

Mechi nyingne iliyochezwa jana ni Bayern Leverkusen 1 vs 0 Atletico Madrid.Gori la pekee hilo lilifungwa na Guilherme.

"POLE CHRIS BROWN MWENZAKO NILICHEKWA "- OMMY DIMPOZ

Msanii Omary Nyembo alimaarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kusema kuwa watu wa uhamiaji duniani kote huwa hawatambui umaarufu wa MTU pindi wanapogundua kuna kitu hakijienda sawa, Ommy Dimpoz amefunguka hayo leo kupitia ukurasa wake wa instagram baada ya mwimbaji kutoka Marekani  Chris Brown kuzuiliwa kuingia Canada na kusababisha kusitishwa kwa show zake mbili alitakiwa kuzifanya Canada ndani ya wiki hii.

Ommy Dimpoz ameonyesha jinsi gani watanzania na mashabiki wake walilipokelea suala lake tofauti na kuonyesha kuwa watu wengi walimcheka na kumchamba kuwa yeye ni mtu maarufu  hivyo asingeweza kupatwa na suala hilo.

"Pole braza Kristofa, haya ni mambo ya kawaida Ila mwenzio nilivyozuiwa kuingia nchini kwenu basi nilivyorudi kwetu nimechekwa ,nimechambwa khaa,hawajuagi mambo ya Uhamiaji hawajali we nani"

Wiki ya wapenda nao msanii Ommy Dimpoz alirudishwa Tanzania baada ya kuzuiwa kuingia Marekani kwa kosa vibali vinavyomruhusu kuingia nchi hiyo kufanya  show.

DEMU KUTOKA KENYA TIARA ANAYEMTAKA KIMAPENZI DIAMOND AINGIZWA MKENGE NA DIAMOND PLATNUMZ

Demu wa Kenya anayejulikana kama TIARA ambae alishindwa kuficha hisia zake na kuntumia video na picha za mitego Diamond kwa kupitia WAKEREKETWA  ametuhabalisha Kuwa baada ya video na picha kusambaa akitafutwa na Diamond platinumz na kuanza kuchati nae na kutumiana picha mbalimbali  na alifikia mahala akasema anamtumia Ticket za kuja Dar wafanye yao pamoja na collabo ya Mziki..Lakini mpaka leo Tickets hazijatumwa..sasa baada ya tickets kutotumwa na Diamond kukaa kimya ilibidi aanza kufanya uchunguzi kuhusu huyo Diamond na mwisho kugundua anachati Diamond Fake..anatumia jina Diamond kwenye Facebook anajiita: DIAMOND WASAFI PLATNUMZZ

Hizo hapo chini ni baadhi ya meseji walizokuwa wanachat kabla ya kugundua sio Diamond wa ukweli.

TIARA amesema bado hajakata tamaa anasema Diamond kama anasoma habari hii soon atakuja Tanzania yeye mwenyewe kukutafuta Face to Face mpaka kieleweke.

Katika hatua nyingine TIARA  amesema mwezi ujao ataachia single yake mpya itakayoitwa KUPARTY.

UNAMSHAURI NINI TIARA?

DAVIDO ASEMA HATAFANYA COLLABO NA MSANII YEYOTE MWAKA HUU:

Davido ameweka wazi kuwa mwaka huu hatafanya collabo na msanii yeyote awe anayechipukia au A-list.

Meneja wa staa huyo Kamal Ajiboye,amesema kuwa Davido amekuwa akipokea maombi mengi ya wasanii wakubwa wadogo wakitaka kufanya naye collabo to kea mwaka huu umeanza na zote amezikataa.

Kamal ameongeza kuwa Davido hataki kufanya collabo yoyote ili kuweka nguvu katika album yake mpya inayotarajiwa kutoka mwezi July,2015.

"The truth it does not take much to feature Davido on any song,but he's seriously working on his album and he has made every member of the team to understand why he won't be welcoming any collaboration for now" Jamal aliiambia Tribune.

DIAMOND APONDWA KUSAFIRI NA KUNDI KUBWA LA WATU KWENYE SHOW AMA SAFARI ZAKE ZA KISTAREHE.

Blogger mmoja maarufu amemshukia na kumshauri Diamond kuhusu kusafiri na kundi kubwa la watu wasiokuwa na ulazima pale anapoenda kufanya show ama starehe.

Ameandika hivi:-

"Anyways, wewe kama mtanzania unaonaje hizi swagga mpya za Diamona kusafiri au kufatwa nyuma na kundi kubwa watu  wakiwemo mameneja wake,ndugu,mpiga picha etc....
Kwa maoni yangu naona kama mameneja wake kama wanampoteza tu,itakuwa kaambiwa akitaka kuonekana  ni big star lazma awe anafatwa nyuma na kundi kubwa la watu everywhere he goes,,,Nimemuelewa kidogo sababu lambda kaona mastaa wakubwa duniani huwa wanakuaga na entourage kubwa ila jamani they can afford kuwa na watu wote wale..some of them make over 10 million dollars a year sasa kulipa watu wote hao  kumfatafata ni pocket change kwake. Tayari wana utajiri ambao hata wajukuu Zhao watakuja kuukuta,wana majumba in every city wengine mpaka Palm Jumeirah  Dubai wana mavacation home sasa huyu kijana wetu ambae mpaka leo anaishi kwenye nyumba ya kupanga,kwanini analipa watu kumfata fata nyuma hivi? Wakati its very unnecessary"

Je wewe unaonaje kuhusu hili swala?

WASTARA AZIMIA KISA PENZI LA BOND

Diva wa filamu nchini,Wastara Juma ambaye sasa anaripotiwa kuwa katika mapenzi na mwigixaji mwenzake, Bond Bin Suleiman anadaiwa kupoteza fahamu Mara tu baada ya kupewa taarifa kuwa mpenziwe huyo amepata mtoto wa nne kwa mwanamke mwingne.

Kwa mujibu wa chanzo makini, Wastara aliyepenyezwa ubuyu na mpenzi wa zamani wa Bond,Lulu Semagongo"Aunt lulu" na kuambiwa kwamba asijishebedue kwani Bond ana mwanamke mwingne am aye amejufungua mtoto wa nne hivi karibuni.

"Tunakushangaa unavyojunadi kwa Bond ni wako na kumpa zawadi ya keki ya birthday wakati mwenzako amezaa na mwanamke mmoja baamedi hivi karibuni.Tena si kwamba mtoto huyo ni wa kwanza ,ni wa nne" kilisema chanzo hicho kikimnukuu Aunty.

Chanzo hicho kifunguka kuwa,baada ya kupewa taarifa hizo na Aunty Lulu,alizimia ghafra na kulazwa hospitali
              " wastara alizimia punde tu baada ya kupewa taarifa hizo,nasikia walimkimbiza hospitali,akapewa huduma,ishu ilikuwa mbaya,Aunt Lulu alimchana live"

Risasi lilimtafuta Aunty Lulu ambaye awali alikuwa akilalamika penzi la kitumwa la kupigwa mara kwa mara na Bond na hata kufikiria mahali na kushukuru Mungu kwa kutengana kwao na kumuuliza kama habari hizo zilikuwa na ukweli wowote.

"Ni  kweli nilimwambia kila kitu Wastara na tulipanga kwenda kumuona mtoto aliyezaliwa ili kujua kama kweli ni wa bond.

"Mimi niliamua kufunguka baada ya Bond kunitukana na kunitolea maneno mazito kwani nilichoka kama amepata presha na kulazwa hilo mi sijui," alisema Aunt lulu.

Kwa upande wake,Wastara alikiri kupoteza fahamu na kulazwa hosptalini,lakini akakataa mambo hayo kumtokea kwa sababu ya jusikia taarifa hizo,bali kutokana name kuzidiwa na malaria.

"Nimepata nafuu na nimeshatoka hospitali nilikuwa ninepatwa na homa kali ya malaria, madaktari waliniambia nilikuwa na malaria 10 kwa muda wa wiki 2 nilikuwa naumwa,lakini nikszidiwa kidogo,hivi sasa niko uwanja wa ndege nashuka nikitokea Mwanza"alisema Wastara

Tuesday, February 24, 2015

SHILOLE NA MCHUMBA WAKE NUH MZIWANDA WACHAFUA HALI YA HEWA MTANDAONI BAADA YA KUTUPIA PICHA ZA UCHI.

Mwigizaji na mwanamuziki,Zuwena Mohammed"Shilole"ambaye ni mama mwenye watoto wawili wa kike,akiwa na mchumba wake Nuh wamechafua hali ya hewa baada ya kutupia picha yao wakiwa uchi.

Nuh mziwanda ndio aliobandika picha hiyo kwenye ukurasa wake kwenye mtandao wa instagram na baada ya kuona watu wengi wanamshambuliaa aliamua kuibandua.

Wapo walioona kuwa kitendo alichokifanya mziwanda labda ni kutokana na umri wake hivyo hayo ni baadhi ya matokeo ya kuwa na mahusiano na mtu mtoto.

Lakini pia wapo walioona kuwa wawili hawa wanatafuta KIKI tu ili media za hapa Bongo ziwazungumzie kama Zari na Diamond,ila pia wapo ambao wanaona hii iko poa na haina tatizo.