Popular Posts

Popular Posts

Popular Posts

Popular Posts

Search This Blog

Popular Posts

Popular Posts

Wednesday, March 4, 2015

ASKARI POLISI WA KIKE AVULIWA NGUO NA KUACHWA MTUPU BAADA YA KUFUMANIWA NA MUME WA MTU,WATU NANE WAFIKISHWA KORTINI.

Wafanyabiashara watatu,na watano wanepandishwa kizimbani katika Mahakama  ya Hakimu Mkazi Singinda wakikabiliwa na mashitaka ya kumdharirisha kupindukia askari polisi wa kike na kumsababisha maumivu makali mwilini

Mwanasheria wa serikali  Petrida Mutta alidai mbele ya Hakimu Joyce Minde kwamba kwa pamoja eashitakiwa  hao walimfanyia unyama askari huyo na kumvua nguo zote na kumwacha mtupu kisha kumshambulia na kusababisha maumivu makali mwilini.

Washitakiwa ni Jasmini Idd (40), Abdalah Handini (26), Ramadhani Bakari (32) wote ni wafanya biashara mjini hapa pamoja na dereva Said Said (50) wengine ni Aurelia Adolf Mushi (20), Grace David Paul (21), Happiness Kiluvya (23), Jackline John (20), Consolata Masaki (21) wote wanadaiwa ni wanafunzi wa elimu ya juu (chuo) cha mkoani hapa Singida.

Mwanasheria wa Serikali alidai wakati wote kitendo hicho cha udhalilishaji  Polisi huyo alikuwa akichukuliwa  picha za video huku akiwa mtupu na kuzisambaza mitandao ya kijamii.

Tukio hilo linadaiwa lilifanyika Februari 14 mwaka huu,saa 11:30 jioni amabako kwa mujibu wa mwendesha mashtaka inadaiwa Polisi huyo wa kike alikutwa akiwa  name mume wa mshitakiwa Jasmin wakiwa kando ya ziwa Singidani wakijivinjari siku ya wapenda nao.

Mutta alidai mbele ya Mahakama  Kuwa kitendo walichofanya washitakiwa ni kinyume cha kanuni ya Adhabu 138A kifungu cha 16, cha mwenendo wa makosa ya jinai.

No comments:

Post a Comment