Popular Posts

Popular Posts

Popular Posts

Popular Posts

Search This Blog

Popular Posts

Popular Posts

Tuesday, March 3, 2015

CHADEMA KILOSA WAMJIA JUU WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimemjia juu waziri Mkuu Mizengo Ponds,kikidai mauaji na maafa ya wakulima na wafugaji ,Mbigili na Mabwegere yametokana na serikali kupitia kwa Pinda kutomsikiliaa aliyekuwa mwanasheria mkuu Jaji Frederick Werema.

Akihojiwa na Tanzania Daima jana,mwenyekiti wa tawi la CHADEMA Mbigili,Maftaha Hamis,alisema CHADEMA kimepokea kwa masikitiko,kuona mauaji na maafa ya wakulima na wafugaji,Mbigili na Mabwegere yanatokana na Pinda kutomsikiliza jaji Werema.

Ndani ya Barua ya Werema aliyomwandikia  Pinda gazeti limefanikiwa  kuona alisema; amebaini uhalali wa kijiji kinachojiita Mabwegere ( usajiri Na 32758 wa 8/12/198 )  una shaka kwasababu kilipata HATI MILIKI ardhi miaka 10 kabla ya kuanzishwa. Hati Na MG/KJJ522 ya JUN 16 1999.

Hamis alidai ' katila barua ya AG Kumb AGC/ 9.20/19/162 ya 1.8.2014 siku chache kabla ya maafa ya kuchomwa moto nyumba 40, ikifuatiwa na vifo vya wakulima wawili na mfugaji mmoja,Werema alimwandikia Pinda akisema
"Nina shauri hatua hizo zichukuliwe haraka"

Kwenye uchambuzi wa Kesi za hukumu ya Mahakama kuu na Mahakama ya Rufaa kuhusu  mgogoro wa Ardhi kati ya kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani,AG alitaja
" mambo muhimu aliyogundua juu ya hukumu hizo,zilizosababisha damu za watu kumwagika na mali kupotea"

i/ Mahakama haikutoa uamuzi wowote kuhusu uhalali wa kuanzishwa kwa kijiji cha Mabwegere .

ii/ Mahakama haikuilekeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kuipa hadhi ya kijiji ,kijiji cha Mabwegere  jukumu hilo si lake.

iii/ Mahakama iliamua kwamba ,Hati ya kumiliki Ardhi iliyotolewa kwa kinachoitwa kijiji cha Mabwegere ni hati halali.

Aisha Werema alisema kumbukumbu zinatoa tafsiri kwamba kijiji cha Mabwegere  kilimilikishwa Ardhi miaka 10 kabla ya kuanzishwa kwake. Kisheria  kijiji au mtu asiyekuwepo hawezi kumiliki Mali  ikiwa ni pammoja na ardhi,hivyo kijiji cha Mabwegere kumilikishwa Ardhi Kabla ya Kuanzishwa kwake kunatia shaka.

No comments:

Post a Comment